• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 9:35 PM
EABL yalenga kuunda lita milioni 100 za ‘Keg’ Kisumu

EABL yalenga kuunda lita milioni 100 za ‘Keg’ Kisumu

Na BERNARDINE MUTANU

Ufanisi wa kiwanda cha pombe Kisumu kilichozinduliwa na Kampuni ya EABL utategemea uzinduzi wa vilabu vya pombe takriban 4,000 eneo hilo.

Kiwanda hicho kitakachogharimu kampuni hiyo Sh15 bilioni kinatarajiwa kukamilika Julai mwaka 2019 na kinalenga kuwapa kazi wasambazaji.

Kampuni hiyo ilizindua kiwanda hicho kwa lengo la kutengeneza pombe aina ya KEG ambayo ni pombe ya bei ya chini.

Kiwanda hicho kitaajiri wafanyikazi 100 moja kwa moja huku idadi ya wakulima watakaokisambazia miwa wakiongezwa hadi 30,000.

Kiwanda hicho kinalenga kutengeneza lita milioni 100 za KEG kila mwaka.

You can share this post!

Kibarua kizimbani kwa kuteka nyara msichana na kumpapasa...

Uwanja wa JKIA watambuliwa kwa ubora Afrika

adminleo