• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Mnangagwa aachia naibu wake mamlaka akianza likizo ya siku 23

Mnangagwa aachia naibu wake mamlaka akianza likizo ya siku 23

Na MASHIRIKA

HARARE, ZIMBABWE

RAIS wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa amemkabidhi makamu wake mamlaka ya kuendesha nchi kwa siku 23 huku akienda likizoni.

Mnangagwa alianza likizo yake Ijumaa na atarejelea mamlaka yake Februari 5, 2022.

Naibu wa Rais Constantine Chiwenga ambaye pia ni Waziri wa Afya, ataendesha nchi kwa muda huo ambao Rais Mnangagwa atakuwa likizoni.

“Wakati huo ambao Rais atakuwa likizoni makamu wa rais Chiwenga atakuwa kaimu rais,” ikasema taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Rais na Baraza la Mawaziri Misheck Sibanda.

  • Tags

You can share this post!

Uhuru mbioni kuwapatanisha Raila, Museveni

Raia wa Congo anayeshtakiwa kwa ulaghai wa Sh105Milioni...

T L