• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 10:08 PM
Mkenya afumaniwa akimbaka ajuza mgonjwa Amerika

Mkenya afumaniwa akimbaka ajuza mgonjwa Amerika

Na PETER MBURU

MWANAMUME Mkenya wa miaka 44 ametiwa mbaroni Marekani, baada ya kupatikana akimbaka ajuza mgonjwa wa miaka 72.
Bw Thomas Kamau Ng’ang’a ambaye ni muuguzi alipatikana na mhudumu mwenzake wa afya akitekeleza unyama huo hospitalini ndipo akaripotiwa.
Bw Ng’ang’a alikuwa muuguzi katika hospitali ya Lexington Rehabilitation and Healthcare, katika eneo la Richmond, Virginia.
Alipatikana akijilazisha ndani ya ajuza ambaye alikua amefika katika hospitali hiyo kutafuta huduma za afya.
Punde baada ya kukamatwa, mshukiwa alizuiliwa jela ya kaunti ya Henrico ambapo alinyimwa bondi, huku akisubiri kufikishwa kortini Desemba.
Aidha, alifutwa kazi mara moja wakati alipokamatwa.
Nakala za korti zilionyesha kuwa Bw Ng’ang’a ana mke na watoto.

You can share this post!

PICHA: Nderemo nje ya mahakama baada ya Obado kuachiliwa

#HurricaneWilla yazua uharibifu Mexico

adminleo