• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:50 AM
Wandani wa Ruto wakashifu mahasimu kutoa ushahidi mpya kuhusu ICC

Wandani wa Ruto wakashifu mahasimu kutoa ushahidi mpya kuhusu ICC

GRACE GITAU Na VALENTINE OBARA

WANDANI wa Naibu Rais William Ruto, wamedai mahasimu wake ndio wanapeana ushahidi mpya kwa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kuhusu ghasia za baada ya uchaguzi wa 2007.

Hivi majuzi, iliibuka mahakama hiyo ingali inakusanya ushahidi kuhusu ghasia hizo ambapo Bw Ruto na Rais Uhuru Kenyatta walikuwa miongoni mwa washukiwa wakuu.

Hii ni licha ya kuwa kesi zao zilisitishwa baada ya kupatikana hapakuwa na ushahidi wa kutosha kuthibitisha walihusika kuchochea au kufadhili ghasia hizo.

Huku ikihofiwa kwamba ufufuzi wa kesi hizo unaweza kumharibia Bw Ruto nafasi kushinda urais 2022, wandani wake jana walidai ripoti hizo kutoka kwa ICC nchini Uholanzi ni njama ya mahasimu wake.

“Ulipelekwa Uholanzi pamoja na Rais, ukashinda. Bado utaibuka mshindi na hatimaye utakuwa rais wetu,” akasema Mbunge wa Tetu, Bw James Gichuhi.

Alizungumza alipoandamana na Bw Ruto na viongozi wengine kwa ibada katika Kaunti ya Nyeri Jumapili.

You can share this post!

Wabunge Rift Valley wamtaka Ruto aache kuwa kigeugeu

Maswali yaibuka kuhusu kimya cha ziara za rais

adminleo