Kimataifa

Mdahalo wa wagombea wenza wa urais Amerika watawaliwa na mapigano Mashariki ya Kati

Na MASHIRIKA October 2nd, 2024 Kusoma ni dakika: 1

SENETA wa Amerika, JD Vance, mgombea mwenza wa Donald Trump, alishindana vikali na Gavana wa Minnesota Tim Walz, ambaye ni mgombea mwenza wa Kamala Harris katika mdahalo wa televisheni ya kitaifa siku ya Jumanne.

Mdahalo huo huenda ukawa wa mwisho uchaguzi wa Novemba 5 ukikaribia.

Mdahalo huo ulitawaliwa na mapigano yanayoendelea Mashariki ya Kati.

Kando na hayo, Walz alionekana akikwepa kujibu baadhi ya maswali na badala yake kumkosoa Trump.

“Cha msingi hapa ni kwamba uongozi thabiti utakuwa muhimu,” Walz alisema.

Baadhi ya mashiriki hata hivyo yanaeleza kuwa Vance aliweza kujieleza kikamilifu katika mdahalo huo.