Babu Owino ni miongoni mwa viongozi waliojiunga na maandamano ya Gen Z
MBUNGE wa Embakasi Mashariki Babu Owino ni miongoni mwa viongozi wa kisiasa ambao Jumatano walioungana na maandamano ya Gen Z kuadhimisha mwaka mmoja tangu mauaji ya wenzao Juni 25, 2024.
Waandamanaji hao walimpokea kwa furaha katika makutano ya barabara za Moi na Haille Sellasie jijini Nairobi, huku wakibeba juu kwa juu.
Mamia ya vijana waliimba, “Babu! Babu! ……..Jawabu ni Babu!” huku wakimchangamkia mbunge huyo machachari.
Baada ya dakika kadhaa Mbunge huyo wa chama cha ODM, japo anayepinga serikali jumuishi, aliingia katika gari lake nyeupe aina ya Prado na kuondoa.
Mnamo Jumanne, Juni 24, 2025, Bw Babu aliwataka vijana kuendelea shughuli za kuadhibisha mwaka mmoja tangu zaidi ya Genz 6 walipouawa kwenye makabiliana kati yao na polisi.
“Kile ambacho nataka kueleza ndugu na dada zangu wa Gen Z ni kuendelea na mipango yao. Niko nanyi na ninawaonga mkono kwa zaidi ya asimilia 100,” akasema.
Awali, Juni 25, 2025, wanasiasa wa upinzani wakiongozwa na Kalonzo Musyoka pia walijitokeza wakisema wanaunga mkono wito wa Gen Z na wazazi wao kuitisha haki