Kimataifa

Chad kutuma wanajeshi 1,500 nchini Haiti punde baada ya polisi wa Kenya kuondoka

Na REUTERS April 22nd, 2026 Kusoma ni dakika: 1

N’DJAMENA, Chad:

CHAD sasa inapanga kuwatuma wanajeshi 1,500 kusaidia kurejesha amani Haiti, taifa ambalo limetawaliwa na magenge.

Afisi ya Rais iliandika barua kwa wabunge Jumatatu kuwa wanajeshi hao watakuwa wakitumwa kuwapiga jeki wale wa Umoja wa Mataifa (UN).

Idadi ya wanajeshi wote Haiti inatarajiwa kufikia 5,500 kufikia mwezi wa nane. Barua hiyo ilisema kuwa tayari wanajeshi 400 wapo Haiti baada ya kutumwa mwezi uliopita pamoja na kiongozi wao.

Chad imefafanua kuwa wanajeshi watakaotumwa upya, watatumwa kwa mikumbo miwili ambapo ni wanajeshi 750 kila mkumbo ndani ya miezi 12.

Awali maafisa 1,000 walikuwa wametumwa wengi wakiwa ni polisi kutoka Kenya lakini pia kulikuwa na wanajeshi wachache kutoka mataifa ya Kati mwa Amerika na Caribbean.

Baraza la Usalama katika Umoja wa Kitaifa iliidhinisha vikosi kutumwa Haiti mnamo Oktoba 2023.

Wanajeshi waliotumwa tayari wamekuwa wakipambana na makundi ya ujangili Haiti ila bado vikosi vingi havijatumwa na mataifa yaliyoahidi kufanya hivyo.

Tangu Oktoba 2023, idadi ya raia wa Haiti ambao wamelazimika kuhama makwao kutokana na ghasia imepanda kutoka 133, 600 huku maelfu ya watu wakiuawa.

Magenge hayo bado yanadhibiti sehemu kubwa ya Haiti hasa mashambani na mijini.

Ukosefu huo wa udhabiti umesababisha Haiti kuahirisha uchaguzi wake mara kwa mara kwa kuwa nchi hiyo iliandaa uchaguzi mara ya mwisho miaka 10 iliyopita.