Habari

Mbunge anayehusishwa na ghasia eneo la Kuresoi asakwa

Na JOSEPH OPENDA na VITALIS KIMUTAI June 22nd, 2026 Kusoma ni dakika: 1

MBUNGE wa Kuresoi Kaskazini, Alfred Mutai bado anasakwa na polisi kwa kuhusishwa na ghasia kati ya wafuasi wake na wale wa Gavana wa Nakuru Susan Kihika wikendi katika eneobunge hilo.

Fujo hizo ziliwaacha watu watano na majeraha ya risasi.

Bw Mutai ni mbunge anayehudumu muhula wa kwanza baada ya kumbwaga aliyekuwa Naibu Spika, Moses Cheboi kupitia UDA mnamo 2022.

Amekanusha kuwa alihusika na ghasia hizo akisema analengwa kisiasa.

Polisi waliwanyaka zaidia ya vijana 56 walioshukiwa kushiriki ghasia katika Shule ya Sekondari ya Umoja, Tulwet.

 

Bi Kihika na wanasiasa kadhaa walikuwa wakiendelea na mkutano wa kuyachangishia makundi mbalimbali kwenye wadi ya Nyota, Kuresoi Kaskazini.

Vijana 44 waliachiliwa huru kutokana na ukosefu wa ushahidi huku 12 wakisalia korokoroni na wanatarajiwa kufikishwa kortini mnamo Jumatatu