• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 1:08 PM
Ubunge umenifanya nitafunwe na uchochole, alia Otiende Amollo

Ubunge umenifanya nitafunwe na uchochole, alia Otiende Amollo

MARY WANGARI Na ANITA CHEPKOECH

MBUNGE wa Rarieda Otiende Amollo Jumanne ameibua ghadhabu mitandaoni baada ya kutangaza kwamba tangu achaguliwe mbunge amekuwa maskini hohehahe licha ya kupokea mshahara wa Sh621,000.

Bw Omollo alisema kwamba tangu alipochaguliwa hajawahi kununua chochote kutokana na uchochole.

Alikuwa akizungumza katika kipindi cha AM Live cha NTV mnamo Julai 9 wakati wa mjadala kuhusu hatua ya wabunge hivi majuzi ya kujiongezea mishahara iliyoibua hisia kali miongoni mwa Wakenya.

Nimekuwa mwenyekiti wa tume ya kupokea malalamishi na pia nimekuwa katika uanasheria usio wa kiserikali. Sijawahi kuwa fukara jinsi nilivyo kama mbunge,” alisema, akiongeza kwamba yeye hupata Sh500,000 licha ya kutokuwa na mkopo wa nyumba.

“Nilipochaguliwa, tayari nilikuwa na nyumba yangu jijini Nairobi, lakini tangu nilipotwaa mamlaka sijanunua nyumba, sijanunua chochote.”

Mwanasiasa huyo alidai kwamba wabunge hutumia mapato yao katika maeneo bunge yao.

Wabunge hupokea kiasi cha Sh250,000 kama marupurupu ya nyumba na wanataka waongezwe marupurupu ya “usiku” kwa jina “Fedha za Matumizi ya Kinyubani” ambapo watapata kati ya Sh18,200 na Sh24,000 kila siku.

Mbunge huyo aliyeonekana kukereka alisema hajawahi kushiriki kikao ambapo wabunge waliitisha nyongeza ya mishahara akisema ilikuwa kazi ya Tume ya Bunge (PSC) katika juhudi za kuwaokoa wanasiasa maskini.

Kulingana na mbunge huyi wa ODM, ripoti za vyombo vya habari za kila mara zilizowasawiri wabunge kama waroho zilisinya na hazikuwa za haki.

“Ukichukua mkopo wa nyumba kwa Sh20 milioni huwezi kuchukua mkop wa gari kwa sababu kiwango kinachokatwa mshahara ni cha juu kwa sababu ya muda mfupo wa kulipa. Nina hakika kuna baadhi ya wenzangu ambao wamechukua mkopo na wanapata sufuri mwisho wa mwezi,” alifafanua  Bw Amollo.

“Hii ndiyo mara ya mwisho nitakayozungumzia swala hili,” alisema.

Wanasiasa wengine wakiwemo Seneta wa Kiambu Kimani Wamatangi, Seneta wa Kericho Aaron Cheruiyot na aliyekuwa Mbunge wa Gem  Jakoyo Midiwo pia walitetea hatua ya kutaka nyongeza ya mshahara huku aliyekuwa Seneta wa Kakamega Boni Khalwale akipinga.

Seneta Wamatangi alifichua yeye hupokea Sh640 pekee baada ya mshahara wake kukatwa.

Mikopo wanayochukua wabunge hukatwa kwenye mishahara yao. Nakala yangu ya malipo sasa imeandikwa Sh640 baada ya kukatwa mishahara.

“Ikiwa sikuwa na biashara, watoto wangu wangeishi katika nyumba lakini hawangekula,” alisema.

Kwa upande wake Seneta Cheruiyot alishangaa wanachofaidika nacho wanahabari baada ya “kuwasawiri vibaya wabunge.”

“Suala tu lenye utata kwa sasa ni kuhusu marupurupu ya nyumba. Leo hii mfanyakazi wa serukali akienda Nakuru watalipwa marupurupu ya kuwastawisha, hakuna kitu ambacho tumewalipa wabunge ambacho hakijalipwa wafanyakazi wengine wa umma,” alisema Bw  Cheruiyot.

Bw Midiwo alisema: “Tatizo la gharama kubwa ya mishahara nchini halitasuluhisha kwa kuondoa mishahara ya watu, linaweza kutatuliwa kwa kukata nyama iliyooza.”

You can share this post!

Neymar akosa mazoezi PSG, tetesi za kurejea Barcelona...

Wizara mbioni kuchunguza dhuluma Nairobi School

adminleo