• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 9:55 AM
Itawabidi Stars kujikakamua zaidi kuzima Comoros na CAR, asema Wanyama

Itawabidi Stars kujikakamua zaidi kuzima Comoros na CAR, asema Wanyama

Na GEOFFREY ANENE

HARAMBEE Stars italenga kujisukuma hata zaidi kupata matokeo mazuri katika mechi zijazo kutokana na motisha ya kunyakua taji la Afrika Mashariki na Kati mwezi Desemba mjini Machakos, nyota Victor Wanyama amesema.

Akizungumza Alhamisi nchini Morocco kabla ya Stars kupimana nguvu na Comoros (Machi 24) na Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR) hapo Machi 27, kiungo huyu wa Tottenham Hotspur amesema, “Tuna motisha kutokana na ushindi wa mashindano ya Cecafa Senior Challenge Cup. Tunataka kuonyesha bidii hiyo na kuendeleza fomu hiyo katika mechi zijazo.”

Wanyama ni mmoja wa wachezaji 16 kutoka nchi za kigeni walioitikia mwito kocha Stanley Okumbi kushiriki michuano hii itakayoathiri msimamo wa Kenya kwenye viwango bora vya soka duniani.

Kenya, ambayo inashikilia nafasi ya 105 duniani, itatumia michuano hii kujipiga msasa kabla ya kupepetana na Ghana katika mechi yake ya pili ya kufuzu kushiriki Kombe la Afrika (AFCON) mwaka 2019.

Vijana wa Okumbi watajipata pabaya kwenye viwango bora vya dunia wakipoteza dhidi ya nambari 132 Comoros na nambari 121 Jamhuri ya Afrika ya Kati.

Mwezi Juni mwaka 2017, Kenya ilizimwa 2-1 na Sierra Leone katika mechi ya ufunguzi ya Kundi F ya kufuzu kushiriki AFCON mwaka 2019. Timu nyingine katika kundi hili ni majirani Ethiopia, ambao waliaibishwa 5-0 na Ghana katika mechi yao ya kwanza.

Kikosi cha Harambee Stars:

Makipa

Patrick Matasi (Posta Rangers), John Oyemba (Kariobangi Sharks), Faruk Shikalo (Bandari)

Mabeki

Harun Shakava (Gor Mahia), Musa Mohammed (FK Tirana, Albania), Brian Mandela (Maritzburg United, Afrika Kusini), David Ochieng, (IF Brommapojkarna, Uswidi), David Owino (Zesco, Zambia), Abud Omar (Slava Sofia, Bulgaria)

Viungo

Patilah Omoto (Kariobangi Sharks), Francis Kahata (Gor Mahia), Duncan Otieno (AFC Leopards), Samuel Onyango (Gor Mahia), Athuman Ismael Gonzales (CF Fuenlabrada, Uhispania), Anthony Akumu (Zesco, Zambia), Victor Wanyama (Tottenham Hotspurs, Uingereza), McDonald Mariga (Real Oviedo, Uhispania), Johanna Omollo (Cercle Brugge KSV, Ubelgiji), Paul Were (FC Kaisar, Kazakhstan), Eric Johana Omondi (IF Brommapojkarna, Uswidi)

Washambuliaji

Ayub Timbe (Heilongjiang FC, Uchina), Cliffton Miheso (Buildcon FC, Zambia), Erick Kapaito (Kariobangi Sharks), Jesse Were (Zesco FC, Zambia), Michael Olunga (Girona FC, Uhispania).

You can share this post!

Pigano la Okwiri na Ouma laahirishwa hadi Aprili 18

Starlets wasalia 108 duniani viwango vya FIFA

adminleo