• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 12:30 PM
Magoha apiga marufuku shughuli zisizo za masomo muhula wa tatu

Magoha apiga marufuku shughuli zisizo za masomo muhula wa tatu

Na CHARLES WASONGA

WAZIRI wa Elimu George Magoha amepiga marufuku shughuli zozote zisizohusiana na masomo wakati wa muhula wa tatu kama sehemu ya mikakati ya kuzuia visa vya udanganyifu katika mitihani ya kitaifa.

Akiongea katika katika Shule ya Wanafunzi wanaoishi na ulemavu ya Machakos, Machakos School for the Physically Disabled Profesa Magoha alisema shughuli za maombi kwa watahiniwa, shule kupokea wageni mbalimbali kwa ajili ya kutoa hotuba za uhamasisho au wazazi kutembelea shule hazitaruhusiwa.

“Na walimu wakuu pia wanaonya dhidi ya kusaidia katika utekelezaji wa wizi wa mitihani au kutowachulia hatua walimu watakaoshiriki uovu huo,” akasema Waziri alipokuwa akikagua shughuli inayoendelea ya mafunzi kwa walimu kuhusu ufundishaji wa mtaala mpya wa umilisi na utendaji (CBC).

“Nafahamu kwamba baadhi ya walimu wakuu wanapanga kuiba mitihani, lakini nawaonya wasithubutu kwani tumeweka mikakati thabiti ya kuhakikisha wanakamatwa,” Profesa Magoha akaongeza.

Waziri huyo pia aliwaonya watahiniwa dhidi ya kushawishiwa kushiriki udanganyifu katika mitihani ya kitaifa ya darasa la nane (KCPE) na ile ya kidato cha nne (KCSE).

“Wale watakaopatikana na hatia ya kuiba mitihani watakamatwa na kusukumwa jela, sawa na wahalifu wengine. Vilevile, matokeo ya wale watakahusika udanganyifu wa mtihani yatafutuliwa mbali,” akasema.

Profesa Magoha alisema kuwa mwezi wa Novemba utakuwa mwezi mahsusi wa mtihani kwani wanafunzi wa madarasa mengine watafunga kwa likizo ndefu mnamo Oktoba 28.

Mtihani wa mwaka 2018 wa KCPE unaanza Novemba 1 na kuisha Novemba 3.

Kwa upande mwingine ule wa KCSE utaanza Novemba 7 hadi Novemba 30, 2019.

You can share this post!

Halmashauri yazindua mkakati wa kuboresha huduma za maji

TAHARIRI: Serikali ijitolee kufaulisha sensa

adminleo