• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 11:55 AM
FUNGUKA: Ninatumia Biblia kuwatafuna mabinti kanisani mwangu

FUNGUKA: Ninatumia Biblia kuwatafuna mabinti kanisani mwangu

Na PAULINE ONGAJI

“Mabinti hawa husikiza wahubiri sana kiasi cha kuwa hawawezi kutambua hata wanapotumiwa kuridhisha kiu cha mtu kimahaba. Wananiandalia maankuli ya kila aina ambapo baadaye wananipa mzinga wa asali chumbani na nikimaliza shughuli nitatoka bila kulipa hata senti. Kupitia rasilmali zao, nina furaha kutangaza kuwa nimeramba zaidi ya nusu ya mabinti kanisani mwangu”

KATIKA ulimwengu wa sasa ambapo kumekuwa na shaka kuhusu maadili ya baadhi ya viongozi wa kidini, Jeremy hajasazwa.

Kaka huyu mwenye umri wa miaka 36 ni mmojawapo wa mapasta wa vijana katika kanisa moja mitaani. Kimaumbile, Jeremy ameumbwa kiasi kwamba utadhani kuwa alichangia mawazo Maulana alipokuwa akimuumba.

Kaka huyu ana umbo la kupendeza huku mazoea yake ya kufanya mazoezi kila mara yakihakikisha kuwa misuli yake inajichora kwa kila vazi analovaa.

Rangi yake ya lami imemfanya kuwa kivutio cha mabinti wengi huku vibonyo vinavyojitokeza kidevuni mwake kila anapotabasamu zikiwaacha mabinti wachanga na akina mama waliokomaa kuduwaa.

Isitoshe, kataalumika ajabu. Jeremy amesomea udaktari lakini ameamua kuacha taaluma yake hiyo ya hali ya juu na kujitosa katika uhubiri. Kinyume na baadhi ya wanaojitosa katika huduma hii kama mwito, sababu zilizomsukuma Jeremy kwa uhubiri ni za kustaajabisha.

“Hii ni mojawapo ya sehemu ambapo una uwezekano mkubwa wa kurambaramba mabinti pasipo gharama. Kuanzia kwa wanakwaya, hadi kwa chama cha vijana na hata wake za watu umehakikishiwa uhondo.

Mabinti hawa husikiza wahubiri sana kiasi cha kuwa hawawezi kutambua hata wanapotumiwa kuridhisha kiu cha mtu kimahaba.

Nalenga hawa mabinti wasio na uhakika kuhusu maisha yao tena wasiojithamini. Hawa ni rahisi sana kuwanasa kwani ninachohitaji ni kuwaonyesha tabasamu na nia ya kuwapenda na sitakumbana na pingamizi yoyote.

Maumbile na sura yangu ya kupendeza pia ni kivutio kwa hao wanaojidai kuwa wa haiba ya juu. Naam wajua wale warembo kupindukia na maumbo ya kupendeza, vile vile taaluma za hali ya juu ambao nia yao huwa kujionyesha kanisani?

Lakini ukwasi wangu katika mahubiri pia kaniongezea alama kibao. Ni halua kwa wanaojifanya watakatifu sana. Ninachohitaji kufanya ni kuwapa deti kwa kisingizio kuwa tutajadili masuala ya dini na kabla hajatanabahi azma yangu, huwa nishamuingiza boksi na kumtafuna.

Kadhalika kuna wake za watu wanaovutiwa na sifa hizo mbili za utanashati na ukwasi wa kuhubiri ambapo mara nyingi mimi ndiye ninayenufaika hata baada ya kutafuna.

Ninachohitaji kufanya ni kumpigia mhusika simu na kumwambia kuwa siku hiyo nitamtembelea kwake kwa maombi. Mara nyingi nafanya hivyo siku za kazi kumaanisha kuwa sio rahisi kunaswa na waume au wapenzi wao.

Isitoshe, ninaposema kuwa naja mimi hupokea pesa za petroli au nikichukua teksi, inalipwa pindi ninapofika ninakoenda.

Nikifika nakutana na maankuli ya kila aina ambapo baadaye nitaandaliwa asali chumbani na nikimaliza shughuli nitatoka bila kulipa hata senti. Badala yake ni mimi nitakayepokea pesa za kunirejesha kwangu.

Kupitia rasilmali hizo, nina furaha kutangaza kuwa nimeramba zaidi ya nusu ya mabinti kanisani mwangu, na bado sikomi huku lengo langu likiwa kuacha alama kwa kila binti anayeingia kwenye jengo hilo”.

You can share this post!

TAHARIRI: Miguna hakustahili kudhalilishwa JKIA

Matiang’i, Kihalangwa na Boinnet waitwa kortini...

adminleo