• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 7:20 PM
Orengo ataka Miguna aundiwe pasi maalum ya usafiri apelekewe Dubai

Orengo ataka Miguna aundiwe pasi maalum ya usafiri apelekewe Dubai

Wakili na Seneta wa Siaya James Orengo. Picha/ Maktaba

Na RICHARD MUNGUTI

MAHAKAMA kuu iliaombwa Alhamisi iamuru Idara ya Uhamiaji itengeneze pasi ya kusafiria ya wakili Miguna Miguna apelekewe Dubai na mawakili Nelson Havi na Aulo Soweto.

Wakili James Orengo ambaye ni mmoja wa mawakili 14 wanaomtetea Miguna aliyedungwa dawa ya kumfanya apoteze fahamu aliambia mahakama sheria inamruhusu mkurugenzi wa idara ya uhamiaji kumtayarishia  mlalamishi cheti maalum cha kusafiria.

“Naomba hii mahakama imwamuru mkurugenzi wa idara ya uhamiaji Bw Gordon Kihalangwa amtengenezee Miguna pasi ya kusafiria kama alivyoamriwa apelekewe Dubai na mawakili Havi na Soweto,” Jaji George Odunga aliombwa na Seneta Orengo.

Jaji Odunga alimweleza wakili huyo mwenye tajriba ya juu kwamba Jaji Enoch Mwita aliamuru Bw Kihalangwa amtayarishie pasi maalum ya kusafiria kutoka Canada.

Pasi ya Kenya aliyokuwa amepewa Miguna ilitwaliwa na Serikali na kufutiliwa mbali.

You can share this post!

Wakili Mutinda aponea kusukumwa jela kwa kuwa...

Iweje Kenya impeleke Miguna Dubai akateseke kama yatima?...

adminleo