• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 3:53 PM
Vyoo vijengwe ufuoni msimu huu wa likizo, wakazi Mombasa wasema

Vyoo vijengwe ufuoni msimu huu wa likizo, wakazi Mombasa wasema

Na DIANA MUTHEU

WAKAZI wa Mombasa wameomba vyoo vya umma vijengwe na vingine viongezwe katika fuo za bahari hasa msimu huu wa likizo.

Wafanyabiashara katika fuo hizi walilalamika kuwa wageni wanaozuru maeneo hayo wanachafua mazingira kwa kuenda haja kubwa na ndogo kwenye vichaka na mawe yaliyo kwenye ufuo.

Fuo za umma katika kaunti ya Mombasa ni kama vile Mombasa, Nyali na Jomo Kenyatta (Pirates).

Uchunguzi wa Taifa Leo ulionyesha kuwa ufuo wa umma wa Jomo Kenyatta ndio pekee una vyoo na viko mita 100 kutoka kwa bahari.

Akizungumza na Taifa, mwanachama wa kikundi cha waokoaji katika ufuo wa Jomo Kenyatta, Hamis Abdallah alisema kuwa vyoo hivyo ni vichache na haviwezi kukidhi mahitaji ya wageni wanaotembelea ufuo huo.

Kutumia vyoo hivi, mja anapaswa kulipa Sh10. Bw Abdallah aliongeza kuwa watu wenye ulemavu hawawezi kutumia vyoo hivi.

Bilal Yusuf , mwanabiashara katika ufuo wa Nyali alisema kuwa kungekuwa na vyoo vya umma hawangepata changamoto kuokota taka nyingi vikiwemo visodo na vibinda vya watoto.

You can share this post!

Makabiliano mapya baina ya madiwani yatarajiwa Nairobi

Upinzani Bolivia wazima vituo vya habari vya serikali

adminleo