• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 10:08 PM
Polisi wageuka wanyama ghafla wakizima maandamano JKUAT

Polisi wageuka wanyama ghafla wakizima maandamano JKUAT

Na Leonard Onyango

MAAFISA wa polisi waliokuwa wakizima maandamano ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha JKUAT mjini Juja, Kaunti ya Kiambu Jumatatu waliacha kuwa binadamu na kugeuka wanyama wasio na akili.

Katika moja ya video iliyotiwa katika mitandao ya kijamii, polisi wanne wakishirikiana na wahuni wanaonekana wakimkanyaga mwanafunzi wa kike na kumpiga kila sehemu ya mwili, hata kichwani, kwa bakora na mateke akiwa amelala chini.

Mmoja wa polisi hao wanyama alikuwa ameshikilia bunduki na wenzake wakiwa na bakora.

Wengine walimkanyaga na kurukaruka kwenye kichwa chake huku wengine wakimshambulia kwa bakora sehemu zingine za mwili.

Video hiyo imezua hisia kali mitandaoni miongoni mwa Wakenya ambao wanataka maafisa hao wa polisi wasiokuwa na utu wakamatwe, wafutwe kazi kisha wafikishwe mahakamani.

Wanafunzi hao walikuwa wakilalamikia kuzorota kwa usalama katika eneo hilo. Hii ni baada ya wahalifu kudunga kisu mmoja wa wanafunzi alipokuwa akielekea chumba cha malazi.

You can share this post!

Ruto apondwa na mawaziri kwa kumpuuza Rais

Timizeni ahadi zenu, balozi wa Amerika arai wanasiasa

adminleo