• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Polo aliyeokoka afichulia waumini yeye ni mpenziwe mke wa pasta

Polo aliyeokoka afichulia waumini yeye ni mpenziwe mke wa pasta

Na SAMMY WAWERU

KANDARA, MURANG’A

WAUMINI wa kanisa moja mtaani hapa walipigwa na mshangao jamaa aliyeamua kuokoka alipodai alikuwa na mpango wa kando wa mke wa pasta.

Jamaa alimwaga mtama na kuaibisha mke wa pasta huku mumewe akitoka na kupoteza fahamu.

Inasemekana polo alijiunga na kanisa hilo kufuatia ushawishi wa pasta na mkewe kwa kipindi cha mwaka mmoja.

“Pasta na mkewe walikuwa wakialika kalameni kwao kumhubiria aokoke,” alieleza mdokezi wetu.

Siku ya kioja pasta alieleza washirika wa kanisa hilo kuwa alikuwa na ujumbe maalum kwao.

“Leo tumejaaliwa kuwa na mgeni, ni kijana ambaye mimi na mke wangu tumefanya kila tuwezalo kumnusuru kutoka ulevini,” alisema mhubiri huyo akialika jombi kutoa ushahidi.

Jamaa alijitambulisha, na kushukuru mtumishi wa Mungu kwa dhati kwa kumgeuza kuwa kiumbe mpya. Alikuwa mcheshi, ambapo kanisa liliangukia kicheko kutokana na aliyosimulia.

Hata hivyo, kanisa lilitulia kama maji mtungini aliposema ana ujumbe maalum aliotaka ujulikane. “Kusema ukweli nina kila sababu ya kutabasamu na kumshukuru pasta kwa kunikomboa.

Naomba mtumishi wa Mungu unisamehe kwa kuwa nusura nivunje ndoa yako kwa kuwa nilikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mke wako, nilikuwa mtenda dhambi lakini naungama makosa yangu,” alitangaza kalameni.

Waumini walijishika tama, kwa siri iliyofichuka wakifahamu fika kuwa mama huyo alikuwa katika mstari wa mbele kanisani kukashifu usinzi kwenye ndoa.

Pasta alipoteza fahamu na kupelekwa katika chumba maalum ili kufanyiwa huduma ya kwanza. Mkewe alionekana akimwaga machozi na kuomba msamaha kwa kanisa.

…WAZO BONZO…

You can share this post!

Mwaani Girls yang’aa kwenye mashindano ya kitaifa ya...

JAMVI: Wazika tofauti zao kisiasa, masaibu ya Mutua yaanza...

adminleo