• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 12:58 PM
Wakenya wengi wanapenda simu za Tecno – Utafiti

Wakenya wengi wanapenda simu za Tecno – Utafiti

Na CHRIS ADUNGO

KAMPUNI ya Uchina, Transsion Holdings inaongoza kwa mauzo ya simu za mkononi katika soko la Kenya kulingan na utafiti wa hivi majuzi.  

Bradi zake tatu, Tecno, Infinix na iTel ni miongoni mwa tano bora zinazoenziwa na Wakenya kote nchini, kulingana na utafiti wa Consumer Insight.

Kwenye ripoti yake, brandi hizo tatu zina jumla ya asilimia 54 ya simu zote zinazomilikiwa na Wakenya. Mwaka 2016, brandi mbili za kampuni hiyo – Tecno na iTel – zilikuwa na asilimia 34 ya soko la simu nchini.

Kwa watu waliohojiwa katika utafiti huo, asilimia 28 wanatumia simu za Tecno, asilimia 16 simu za Samsung, asilimia 12 Nokoa na asilimia 10 Infinix.

Katika ripoti tofauti, kampuni ya Jumia imeonyesha kuwa Kenya inaongoza kote ulimwenguni kwa trafiki ya intaneti kutokana na ununuzi wa simu na kuipiku Nigeria, ambayo iliongoza mwaka 2017.

Ripoti hiyo pia ilionyesha kuwa kampuni ya Transsion Holdings imechochea pakubwa kupanuka kwa utumizi wa simu za kisasa humu nchini. Kampuni hiyo kutoka Hong Kong ndiyo kubwa zaidi barani Afrika kwa mauzo.

Brandi za simu za Korea Kusini kama Samsung, Huawei, LG  na Nokia zimepata ushindani mkali kutoka kwa brandi za Uchina zinazowapa Wakenya simu za kifahari kwa bei nafuu.

You can share this post!

Shujaa yalemewa na Fiji kwenye fainali

Mke wa mwanamume achukuliwa na mwenzake baada ya kupoteza...

adminleo