• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 11:13 AM
SENSA: Wakenya 20,000 hulala nje penye baridi kila siku

SENSA: Wakenya 20,000 hulala nje penye baridi kila siku

Na PETER MBURU

WATU wapatao 20,101 hulala nje penye kibaridi kila siku kwa kukosa makao, kulingana na takwimu zilizotolewa na Shirika la Takwimu (KNBS), kutokana na sensa iliyofanywa 2019.

Kati ya idadi hiyo, wanaume wanajumuisha 17,747 nao wanawake wakiwa 2,348 huku wanaoishi mijini wakiwa wengi kwa idadi ya 14,581, na wanaoishi mashambani ambao ni 5,520.

Kaunti ambayo haikurekodi kisa cha mtu anayelala nje ni Isiolo pekee, huku Nairobi ikiwa na visa vingi zaidi, vikiwa watu 6,743. Kati ya idadi hiyo, wanaume walikuwa 6,064 nao wanawake 679.

Takwimu za ripoti hiyo zimeonyesha kuwa wanaume wengi ndio wanalala nje, maeneo ambako wanawake wengi walirekodiwa kuwa wakilala nje yakiwa Nairobi (679), Mombasa (230), Kisumu (136) na Migori (103).

Takwimu hizi zimeripotiwa wakati serikali inaendeleza mpango wa kutengeneza nyumba za gharama nafuu, kwa lengo la kuhakikisha kuwa kila Mkenya anaishi katika mazingira nadhifu.

Vilevile, zimetolewa wakati tatizo la familia za mitaani limekuwa likisumbua mashirika ya serikali na serikali nyingi za kaunti.

, huku washikadau wakijaribu mbinu za kumaliza familia hizo.

Wakati wa kufanya hesabu hiyo, watu ambao walikuwa katika vituo vya matibabu ama kuelimishwa hawakuhesabiwa, ila ni waliokuwa mitaani pekee waliohesabiwa.

You can share this post!

SENSA: Wakenya 14,000 wana umri wa zaidi ya miaka 100

SENSA: Walemavu wengi ni wanawake

adminleo