• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 12:30 PM
Waliotupwa jela kimakosa miaka 36 kufidiwa Sh297m kila mmoja

Waliotupwa jela kimakosa miaka 36 kufidiwa Sh297m kila mmoja

MASHIRIKA Na MARY WANGARI

WANAUME watatu kutoka Baltimore waliokuwa vijana chipukizi walipohukumiwa kifo kimakosa mnamo 1984 wanatazamiwa kupokea Sh297 milioni kila mmoja kutoka kwa mamlaka ya Maryland.

Hii ni kupitia mpango wa malipo uliopendekezwa ambao Bodi ya Huduma za Umma inatazamiwa kupigia kura mnamo Jumatano.

Mpango huo ulifichuliwa katika vipengele vya ajenda vilivyochapishwa na bodi hiyo mnamo Jumatatu.

Alfred Chestnut, Ransom Watkins na Andrew Stewart walikuwa na umri wa miaka 16 kila mmoja wakati maafisa wa polisi mjini Baltimore walipowalenga kama washukiwa katika mauaji ya Novemba 1983 ya mvulalana mwenye umri wa miaka 14 ndani ya Shule ya Upili ya Harlem Park Junior na kupuuza mashahidi kadhaa na vidokezo vilivyoashiria mtu mwingine.

Wakati mawakili wa upande wa washtakiwa walipouliza ushahidi kuhusu mshukiwa huyo mwingine, mwendeshaji mashtaka wa Baltimore alimdanganya jaji na kusema hakukuwa na ripoti kama hizo.

Hatimaye Chestnut ilivumbua ripoti hizo katika maombi ya rekodi za umma lwa mwanasheria mkuu wa Maryland mnamo 2018, akaziwasilisha kwa wakili mkuu eneo la Baltimore, Marilyn Mosby mnamo 2019, na kitengo cha Uadilifu wa Mashtaka cha Mosby kikajitahidi kuwezesha wanaume hao kuachiliwa huru kabla ya Sikukuu ya Thanksgiving — miaka 36 tangu walipofungwa jela kwa mara ya kwanza.

Maryland haina masharti ya kuwafidia washtakiwa waliohukumiwa kimakosa, badala yake huwaruhusu kuwasilisha malalamishi kwa Bodi ya Huduma za Umma, ambayo “huenda ikaruhusu kiasi fulani” lakini kwa miaka mingi haikufanya hivyo.

Lakini mswada umewasilishwa katika Bunge Kuu la Maryland ambao utahitaji bodi hiyo kuwalipa fidia watu waliohukumiwa kimakosa.

Mswada huo unalenga kuwezesha kufidiwa kwa wale waliohukumiwa kimakosa kiasi fulani cha hela kwa kila mwaka ambao walitumika kifungo cha jela

You can share this post!

Papa Francis haugui virusi vya corona – Ripoti

Kimbunga chaua wawili, chaharibu nyumba 40

adminleo