• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 12:58 PM
Kizimbani kwa kuiba maski za Sh950,000

Kizimbani kwa kuiba maski za Sh950,000

Na Richard Munguti

Wafanyabiashara wawili walishtakiwa Ijumaa kwa kumlaghai mfanyabiashara maski zipatao 252 zenye thamani ya Sh957,600.

Mabwana Charles Nyamai Nzivani (kulia pichani) na Benson Mutuku Nzioki walikanusha mashtaka mawili ya kula njama ya kumtapeli Erick Mwiti Gitiye barakoa hizo.

Washtakiwa pia walikabiliwa na shtaka la pili la kupokea bidhaa wakidai walikuwa na uwezo wa kuzinunua.

Walikana walipokea maski hizo za hali ya juu mnamo Aprili 22 2020 jijini Nairobi. Waliomba waachiliwe kwa dhamana.

Hakimu mkazi Daniel Ndungi aliwaachilia kwa dhamana ya Sh300,000 kila mmoja.

Washtakiwa hao waliomba wapinguziwe dhamana hiyo wakisema “ni ya juu na kamwe hawawezi kuipata dhamana hiyo.”

Washtakiwa hao waliomba wapunguziwe dhamama wakidai “mapato yao ni kidogo.”

Akitoa uamuzi Bw Ndungi alisema “dhamana hiyo inalingana na makosa dhidi yao.”

Aliongeza kusema baroko hizo zilikuwa zapelekwa kupewa wataalam wa matibabu wanaopambana kuangamiza gonjwa la Corona.

“Yadaiwa mlimfuja mlalamishi maski ambazo zatumika kuzuia kuenezwa kwa gonjwa la Corona ambalo limekuwa janga,” Bw Ndungi alisema.

Alikataa kuwapunguzia dhamana hiyo na kusema “inalingana na makosa dhidi yao.”

You can share this post!

Makanisa yapeperushe ibada mitandaoni lakini yazingatie...

Mwanamke anayeshtakiwa kumuua mpenziwe azuiliwa

adminleo