• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Jamii ya Wamakonde yalalama imetengwa katika ugavi wa chakula

Jamii ya Wamakonde yalalama imetengwa katika ugavi wa chakula

Na MISHI GONGO

JAMII ya Wamakonde wanaoishi eneo la Makongeni, Msambweni katika Kaunti ya Kwale, ina malalamiko kuhusu kutengwa katika ugavi wa chakula unaoendelea katika kaunti hiyo.

Wanasema japo Rais Uhuru Kenyatta aliitambua jamii hiyo kuwa kabila la 43 nchini, wameendelea kubaguliwa katika ugavi wa misaada ya chakula kinachoendelea kutolewa kuwasaidia wasiojiweza katika jamii kipindi hiki ambapo janga la corona limelemaza shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Baadhi ya wakazi hao wamelalamikia majina yao kutolewa katika orodha ya wanaofaa kusaidika na misaada ya chakula kutoka kwa serikali ya kaunti kwa kile wanachokitaja kuwa ni viongozi kudai kwamba jamii hio haitambuliwi

Maureen Thomas akisikitishwa na jinsi alivyokosa nafasi katika mradi wa kazi mtaani ulioanza siku tatu zilizopita ili kuwapiga jeki vijana wakati huu ambapo taifa linapigana na janga la corona.

Hata hivyo, mzungumzaji wa jamii hiyo aliwataka wakazi hao kuwa na subira shughuli hiyo itakapoendelea.

Awali Gavana wa Kaunti ya Kwale Salim Mvurya aliwahakikishia wakazi wa kaunti hiyo kuwa familia zote zisizojiweza zitanufaika na chakula hicho.

You can share this post!

Waliong’olewa paa kwa kukosa kulipa kodi wapata...

Diwani wa chama tawala aaibika wakazi wa Kariobangi Sewage...

adminleo