• Nairobi
  • Last Updated March 19th, 2024 1:13 PM
Watu wanne wasombwa na maji eneo la Ngoliba

Watu wanne wasombwa na maji eneo la Ngoliba

Na LAWRENCE ONGARO

BAADA ya wakazi wanne kusombwa na maji katika mto Athi, eneo la Ngoliba Thika Mashabiki, wakazi wanaiomba Kaunti ya Kiambu usaidizi.

Mnamo Jumatano wakazi wanne wa kijiji cha Ngoliba walisombwa na maji walipokuwa wakivuka Mto Athi wakiwa kwenye boti.

Wakazi wa eneo hilo walisema ya kwamba walikuwa watu sita katika mashua hiyo lakini wawili miongoni mwao walijinusuru na wakaogelea hadi upande wa pili.

Mnamo Jumatano naibu gavana wa Kiambu Bi Joyce Ngugi alizuru kijiji hicho ambapo aliwahakikishia wakazi kuwa kaunti hiyo itajenga daraja la kuvukia upande wa pili.

Chakula kwa wakazi

Alisema serikali ya kaunti inapanga kusambaza chakula kwa wakazi wa eneo hilo.

Bi Ngugi aliwashauri viongozi waache kuingiza siasa katika shughuli hiyo ya kusambaza chakula.

“Sisi kama viongozi tunastahili kuugana na kusaidia wananchi bila kuegemea upande wowote,” alisema Bi Ngugi.

Alisema kaunti ya Kiambu itafanya juhudi kuona ya kwamba kila mwanachi anapata chakula bila kubaguliwa.

Aliwashauri madiwani, machifu na wazee wa vijiji kuketi pamoja na kupanga vizuri jinsi wananchi wanavyostahili kupewa chakula.

Bi Judy Nyaguthii Wang’ombe, alisema mwanaye wa kiume alisombwa na maji alipoungana wa wenzake watano kwenda kuvua samaki.

Hata hivyo, alisema ilidaiwa mawimbi mazito ndiyo yalisababisha sita hao kusombwa na maji.

Licha ya kikosi cha uokozi kufika eneo hilo kwa juhudi za kuokoa watu hao bado walishindwa kuwapata.

Lakini watu wawili pekee ndio walifanikiwa kujinusuru kutoka kwa mto huo ambao unavuma kwa kasi kubwa.

Alisema kwa muda wa siku tatu mfululizo mvua kubwa imenyesha katika eneo hilo.

Bi Wang’ombe alitoa mwito kwa serikali kuwatafutia ajira vijana wengi ambao hawana kazi ya kufanya.

“Kijana yangu alikuwa ana ujuzi wa kurekebisha umeme, lakini hajafanikiwa kupata kazi,” alisema Bi Wang’ ombe.

Wakazi wa kijiji hicho wanaiomba serikali iingilie kati mara moja kuona ya kwamba daraja la kisasa linajengwa ili watu waweze kuvuka kwa urahisi hadi upande wa pili.

You can share this post!

Mwathethe astaafu kumpisha Kibochi wadhifa wa mkuu wa...

Mafuriko yapoteza maji jiji kuu

adminleo