• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 1:15 PM
Seneta Malala kusimamia mchakato wa kumtetea Waiguru Seneti

Seneta Malala kusimamia mchakato wa kumtetea Waiguru Seneti

IBRAHIM ORUKO

Seneta wa Kakamega Cleophas Malala alichaguliwa kuwa katibu wa wanakamati 11 watakao chunguza kung’olewa mamlakani kwa Gavana wa Kirinyaga Anne Waiguru .

Alichaguliwa bila kupingwa katika mkutano wa kwanza wa kamati hiyo Jumatano asubuhi.

Seneta mteuliwa Abshiro Halake alichaguliwa kuwa naibu katibu wa kamati hiyo. Alipata kura tano huku mwenzake wa Nyandarua , Mwangi Githiomi akipata kura nne .

Senator Malala alisema kwamba kamati hiyo itahakikisha usawa na haki kati ya wanaohusika.

“Tutahakikisha usawa na haki bila mapendeleo; nchi yote inatuangalia. Wahusika wote watashughulikiwa kwa usawa,” alisema Bw Malala.

You can share this post!

Wiper, CCM zaingia Jubilee

Rais wa Honduras na mkewe wapatikana na corona

adminleo