IBRAHIM ORUKO
Seneta wa Kakamega Cleophas Malala alichaguliwa kuwa katibu wa wanakamati 11 watakao chunguza kung’olewa mamlakani kwa Gavana wa Kirinyaga Anne Waiguru .
Alichaguliwa bila kupingwa katika mkutano wa kwanza wa kamati hiyo Jumatano asubuhi.
Seneta mteuliwa Abshiro Halake alichaguliwa kuwa naibu katibu wa kamati hiyo. Alipata kura tano huku mwenzake wa Nyandarua , Mwangi Githiomi akipata kura nne .
Senator Malala alisema kwamba kamati hiyo itahakikisha usawa na haki kati ya wanaohusika.
“Tutahakikisha usawa na haki bila mapendeleo; nchi yote inatuangalia. Wahusika wote watashughulikiwa kwa usawa,” alisema Bw Malala.