• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 3:03 PM
Madaktari watoa sindano 7 kutoka tumbo la mtoto

Madaktari watoa sindano 7 kutoka tumbo la mtoto

TITUS OMINDE na DENNIS LUBANGA

MADAKTARI katika Hospitali ya Mafunzo na Rufaa ya Moi (MTRH) mjini Eldoret wamefanikiwa kutoa sindano saba kutoka tumboni mwa mtoto wa miaka mitatu.

Mtoto huyo alilazwa hospitalini humo kutoka katika kaunti ya Pokot Magharibi siku tatu zilizopita.

Upasuaji huo wa saa moja na dakika 45 uliongozwa na Prof Robert Tenge ambaye anasimamia kitengo cha upasuaji watoto hospitalini humo.

Kwa mujibu wa Prof Tenge, sindano sita zilikuwa zimekwama katika maini huku sindano nyingine ikiwa imekwama katika utumbo.

Profesa Tenge alisema historia ya afya ya Dorcas Chepchumba ilionyesha kuwa amekuwa akiishi na sindano hizo za kushona nguo tumboni mwake kwa mwaka mmoja uliopita.

Sindano hizo ziligunduliwa alipolazwa katika hospitali ya kaunti ya West Pokot mjini Kapenguria mapema wiki jana akilalamikia maumivu ya tumbo.

Uchunguzi wa x-ray hospitalini humo ulibaini mtoto huyo alikuwa na sindano tumboni mwake kabla ya kuelekezwa katika hospitali ya MTRH kwa upasuaji.

“Tulipokea mtoto huyo na kumfanyia uchunguzi ambapo tulibaini kuwa alikuwa na sindano tumboni mwake, kabla ya kuanzisha mikakati ya kutoa sindano hizo tumboni humo,” alisema Profesa Tenge.

 

You can share this post!

Mzozo Knut wachacha huku Sossion akitupwa nje

MAKALA MAALUM: Madereva wa kike sasa kivutio kipya katika...

adminleo