• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 2:55 PM
Mhasibu akana kuiba mamilioni ya mwajiri

Mhasibu akana kuiba mamilioni ya mwajiri

Na RICHARD MUNGUTI

MHASIBU mmoja alishtakiwa Jumanne kwa wizi wa Sh8.6milioni.

Bw Stanley Mwangangi Mukinya alishtakiwea kwa kosa la kuiba pesa hizo kutoka kwa mwajiri wake Xylon Motors.

Bw Mukinya alikana aliiba pesa hizo kati ya Novemba 2, 2016 na Septemba 14, 2017.

Mahakama ilifahamishwa na kiongozi wa mashtaka Solomon Naulikha kuwa kesi dhidi ya Mukinya itaunganishwa na nyingine dhidi ya Nancy Waithera Mwangi itakayotajwa Mei 23.

“Naomba korti imwachilie mshtakiwa kwa dhamana sawa na ile ya Bi Mwangi ya Sh300,000 pesa taslimu,” alisema Bw Naulikha.

Hakimu mkuu Francis Andayi alimwachilia mhasibu huyo.

You can share this post!

Idara ya magereza yaagizwa imtengee nafasi mshukiwa mwenye...

Deya aachiliwa kwa dhamana ya Sh10 milioni

adminleo