• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 1:14 PM
Wakenya sasa wachangamkia mashangingi

Wakenya sasa wachangamkia mashangingi

Na BERNARDINE MUTANU

Idadi ya magari ya kifahari yanayonunuliwa imeongezeka kwa asilimia tano katika robo ya mwanzo ya 2018.

Mauzo ya mashangingi hayo yameongezeka katika maduka ya DT Dobie na RMA Kenya ambayo ni 65 ikilinganishwa na 62 mwaka 2017.

Ripoti hii ni kwa mujibu wa takwimu kutoka Chama cha Wauzaji Magari (KMI).

Hata hivyo, mauzo ya magari hayo bado yamo chini yakilinganishwa na magari ya kawaida (mapya) ambayo mauzo yake yaliongezeka kwa asilimia 13.6 kutoka 2,755 hadi magari 3,130.

Mauzo ya magari aina ya Porsce pia yaliongezeka ikiwemo ni pamoja na Porsche Cayenne hadi 22 kutoka matano.

Hii ni kutokana na kampeni kubwa ya mauzo iliyofanywa na Porsche, alisema afisa wa kampuni hiyo.

You can share this post!

UTALII: Mkiendelea kuiga wenzenu mtatimua watalii

Kiwanda kipya cha Coca-cola kupunguza ukosefu wa ajira

adminleo