• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 12:26 PM
Mbunge na mumewe watimuliwa gesti kwa kukosa cheti cha ndoa

Mbunge na mumewe watimuliwa gesti kwa kukosa cheti cha ndoa

Na ANITA CHEPKOECH

MBUNGE Mwakilishi wa Wanawake Kaunti ya Laikipia, Bi Catherine Waruguru na mumewe, mnamo Jumamosi walifukuzwa katika hoteli moja mjini Kericho kwa kukosa kuonyesha cheti chao cha ndoa.

Mumewe Bw Kiprotich Kiget alikuwa amekodisha chumba cha malazi mwendo wa saa kumi jioni katika gesti ya Sunshine kabla ya kuelekea kwao mashambani..

Lakini waliporudi hotelini mwendo wa saa tatu unusu za usiku, wasimamizi waliwakataza kuingia chumbani hadi watoa cheti cha kuonyesha wao ni mume na mke.

Hata juhudi za wabunge watatu wa eneo hilo kupigia simu wasimamizi hao wakiwahakikishia wawili hao ni wanandoa hazikuwafanya kubadili msimamo. Iliwabidi kutafuta hoteli nyingine.

Lakini wasimamizi wa hoteli hiyo walijitetea wakisema walikuwa na haki ya kukataa kuwapa wawili hao chumba cha kulala na ni sheria kwa hoteli hiyo kutoruhusu mwanamume na mwanamke ambao hawajaoana kulala chumba kimoja.

 

You can share this post!

Kioja miili ya mwanamume na mwanamke kupatikana na kondomu...

ICC yafikisha miaka 20 huku ikikosolewa

adminleo