• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Wakili kizimbani kwa kuvunja vikombe na sufuria

Wakili kizimbani kwa kuvunja vikombe na sufuria

Wakili Mohammed Salaani (kulia) akiwa kizimbani pamoja na Bw Osman Godana Jillo na Abdulaziz Hassan Abdullahi waliposhtakiwa kwa kuharibu vyombo. Picha/RICHARD MUNGUTI

Na RICHARD MUNGUTI

WAKILI alishtakiwa kuvunja vikombe na kuharibu sufuria na chakula na kusababishia mkahawa ulioko katika jengo la Jamia, Nairobi hasara ya Sh400,000.

Wakili Mohammed Salaani alishtakiwa pamoja na Bw Osman Godana Jillo na Abdulaziz Hassan Abdullahi mbele ya hakimu  mkuu mahakama ya Milimani Bw Francis Andayi.

Walikanusha shtaka dhidi yao baada Bw Andayi kukataa ombi la wakili Salaani la kusitisha akisomea shtaka. Bw Salaani aliwakilishwa na Bw Muendo Uvyu.

Bw Uvyu alimsihi hakimu asitishe kesi dhidi ya Bw Salaani asuluhishe mambo kadhaa na afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DDP).

“Naomba kesi dhidi ya Bw Salaani iahirishwe kwa muda wa wiki moja asuluhishe mambo kadha na afisi ya DPP,” Bw Uvyu aliomba.

Aliendelea kusema , “ Mshtakiwa huyu ni wakili na hakuhusika na kisa hiki. Naomba kesi dhidi yake iahirishwe hadi asuluhishe mambo kadha na afsi ya DPP.”

Hakimu alimwuliza Bw Uvyu , “Je, si ni afisi ya DPP iliyoidhinisha kesi dhidi ya washtakiwa hawa watatu iwasilishwe kortini?”

“Ndio,” akajibu Bw Uvyu.

“Na je, ni suluhu gani nyingine mshtakiwa anatafuta kama afisi ya DPP ndiyo iliamuru ashikwe na kufunguliwa mashtaka,” Bw Andayi alimhoji wakili.

Hakimu alikataa ombi la mshtakiwa huyo na kuamuru kesi iendelee na kuamuru wasome shtaka dhidi yao.

Walikabiliwa na shtaka la kuharibu mali katika Mkahawa ulioko kwenye Jamia Shopping Mall unaomilikiwa na Bi Aisha Wacuka Wahome mnamo Julai 13 2018.

Shtaka lilisema kuwa watatu hao walivunja , masahani , vikombe, bilauri, masufuria na chakula. Thamani ya mali iliyoahiribiwa ni Sh400,000.

Washtakiwa waliachiliwa kwa dhamana kesi dhidi yao kuorodheshwa kusikizwa Agosti 21, 2018.

“Hata wakishtakiwa bado tutawasilisha mamalamish yetu kwa DPP Bw Noordin Haji,” alisema Bw Uvyu.

  • Tags

You can share this post!

Polo ajuta kutomasa mama pima kazini

Akiri alipokea mamilioni kununulia wanakijiji shamba

adminleo