• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 4:12 PM
Pombe imezuia vijana kuzaa – Gavana Kahiga

Pombe imezuia vijana kuzaa – Gavana Kahiga

Na Stephen Munyiri

GAVANA wa Nyeri, Bw Mutahi Kahiga, amedai upungufu wa watoto wanaojiunga na shule za chekechea umetokana na ulevi wa vijana katika kaunti hiyo.

Bw Kahiga alisema mwaka huu serikali yake iliajiri walimu zaidi ya 700 wa chekechea lakini kuna wasiwasi kwamba idadi ya watoto inapungua.

Akihutubia wananchi katika kituo cha basi cha Karatina baada ya kukagua ukarabati wa barabara, alidai wanaume wengi wamekosa nguvu za uzazi kwa sababu ya unywaji pombe kupindukia.

“Tumejenga shule tukaajiri walimu wa chekechea lakini inasikitisha kuwa hatuna watoto wa kutosha kwa sababu ya unywaji pombe kupindukia.

Hii inahuzunisha. Acheni kunywa pombe kupita kiasi na mzae watoto zaidi,” akasema na kuibua kicheko kutoka kwa umati uliokuwepo.

Bw Kahiga alitoa mfano wa mji wa Karatina ambapo kuna mabaa yanayofunguliwa hata saa mbili asubuhi akaonya kuwa serikali yake itafutilia mbali leseni zao.

Miezi miwili iliyopita, Waziri wa Usalama wa Ndani, Dkt Fred Matiang’i, alipozuru Karatina alionya maafisa wa utawala wa serikali eneo hilo ambao hufumbia macho biashara za pombe haramu na kuwaambia watafutwa kazi.

You can share this post!

Mbunge apinga wazo la kuondoa shule za mabweni

KURUNZI YA PWANI: Kampeni ya kuangamiza unywaji wa pombe...

adminleo