• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 4:10 PM
EACC yaagizwa impe Kidero nakala za ushahidi

EACC yaagizwa impe Kidero nakala za ushahidi

Na RICHARD MUNGUTI

HAKIMU mwandamizi Bw Lawrence Mugambi Jumatano aliamuru Tume ya Kupambana na Ufisadi nchini (EACC) impe aliyekuwa Gavana wa Nairobi Dkt Evans Kidero na washtakiwa wengine 10 nakala za ushahidi katika kesi inayomkabili ya ulaghai wa Sh213 milioni.

Bw Mugambi alitoa agizo hilo baada ya kujulishwa na kiongozi wa mashtaka Bw Alexander Muteti kuwa nakala za mashahidi zitakuwa tayari ifikapo Ijumaa.

Bw Muteti alisema kuwa nakala hizo zaweza kupokewa na mawakili wanaowatetea washtakiwa mnamo Ijumaa.

Bw Mugambi aliamuru kesi hiyo itajwe Agosti 29 mawakili wa washtakiwa waeleze mahakama ikiwa walizipata nakala hizo.

Dkt Kidero na wenzake wamekanusha walilipa kampuni mbili Ngurumani na Lodwar mamilioni hayo bila kutoa huduma zozote kwa gatuzi hili la Nairobi.

Washtakiwa walikanusha mashtaka 34 na wakaachiliwa kwa dhamana ya Sh3 milioni.

You can share this post!

Masaibu ya Sofapaka yaipa Gor ushindi, ubingwa wanukia

EACC yapewa fursa ya mwisho kuwakamata Wakhungu na Waluke

adminleo