• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 11:13 AM
#LewaMarathon kufanyika Juni 30

#LewaMarathon kufanyika Juni 30

Na BERNARDINE MUTANU

Mbio za 19 za Lewa zitafanyika Jumamosi Juni 30, 2018 katika Hifadhi la Wanyamapori la Lewa.

Mbio hizo (nzima na nusu) ambazo zimefadhiliwa na Safaricom zitashirikisha wananchi kutoka mataifa mbali mbali ulimwenguni.

Watakaoshiriki sio lazima wawe wanariadha mahiri, wanaweza kuwa wanariadha wowote wanaotaka kushiriki.

Mashindano hayo hufanyika kila mwaka kwa lengo la kuchangisha kusaidia jamii na kuhifadhi wanyama wa mwituni.

Watakaoshiriki wanaweza kujiandikisha katika tovuti ya hafla hiyo.

You can share this post!

Kenya yapata mkopo mwingine kutoka Ufaransa

Walioshtakiwa kununua rukwama za Sh900,000 warudishwa ndani

adminleo