• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 7:20 AM
Sukari yote yenye nembo ya Mumias ni feki – Ripoti

Sukari yote yenye nembo ya Mumias ni feki – Ripoti

Na BERNARDINE MUTANU 

SUKARI yote yenye nembo ya  Mumias unayoinunua katika maduka ni fekiRipoti hii ni kwa mujibu wa wabunge kutoka Magharibi mwa Kenya. 

Wabunge hao watatu wamedai kuwa sukari ya magendo inapakiwa katika mifuko yenye nembo ya Mumias na kuuzwa kama sukari inayotoka kwa kampuni hiyo. 

Wabunge hao, Godfrey Osotsi (maalum), Caleb Amisi (Sabotina mwakilishi wa kike wa Busia Florence mutua walisema walaghai wa sukari wamebuni njama mpya ya kulemaza zaidi kampuni hiyoambayo haifanyi vyema kwa sasa. 

Baada ya kupakiwasukari hiyo husambazwa kwa maduka ya rejareja kuuzwa maeneo mbali mbali nchini. 

Zaidi, magunia yanamowekwa sukari hiyo hayana siku ya kutengenezwa au ya kuharibika. 

Kwa muda wa miezi sita, kampuni ya Mumias haijatengeneza sukari.

You can share this post!

Wanaofanya biashara na mashirika yasiyo na PIN ya KRA...

Mkurugenzi aliyejiuzulu kusalia ofisini kwa miezi 6

adminleo