• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 6:50 AM
Wakenya washauriwa kuchukua bima ya mazishi

Wakenya washauriwa kuchukua bima ya mazishi

Na BERNARDINE MUTANU

WAKENYA wameombwa kuchukua bima ya mazishi ili kuwafaa zaidi wanapopatwa na msiba.

Shirikisho la Watoaji Bima nchini (AKI) Alhamisi lilitoa ushauri huo kutokana na changamoto za kifedha kubwa ambazo ushuhudiwa wakati wa msiba.

“Kwa kutoa Sh100 kwa mwezi, hili ni suluhu ambalo litahakikisha familia haziachwi taabani kifedha zinapompoteza mpendwa,” alisema Mkurugenzi Mkuu wa AKI, Tom Gichuhi.

Kwa sasa, ni asilimia tatu ya Wakenya ambao wamechukua bima ya mazishi kulingana na utafiti uliofanywa na Ipsos Synovate.

Utafiti huo ulifanywa miongoni mwa makundi 10 Nairobi, Kisii, Kisumu, Nyeri na Bungoma. Ulionyesha kuwa gharama ya mazishi imeendelea kuongezeka.

Walioshiriki walilalamika kuwa mazishi yamefanywa suala la kibiashara ambapo hafla huandaliwa kwa kati ya Sh50, 000 na Sh300, 000.

Familia ambazo huzika wapendwa wao katika kipindi cha siku moja hutumia takriban Sh10, 000.

Wakati marehemu ameaga dunia akiwa hospitalini, familia hutumia kati ya Sh400, 000 na Sh2.5 milioni na kutatiza familia zilizoachwa kifedha.

You can share this post!

KCB yatuza timu yake ya raga kwa kugaragaza washindani

Kidero apinga kushtakiwa upya

adminleo