• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 3:04 PM
Walioiba pesa za NHIF wanastahili adhabu ya wauaji, asema DPP

Walioiba pesa za NHIF wanastahili adhabu ya wauaji, asema DPP

NA RICHARD MUNGUTI

MKURUGENZI wa Mashtaka ya Umma (DPP) Noordin Haji alieleza mahakama ya kuamua kesi za ufisadi kuwa wakuu 21 katika hazina ya kitaifa ya bima (NHIF) walifanya makosa mabaya sawa na ya kuua kwa kuiba pesa za kufadhili matibabu ya wagonjwa kote nchini.

“Naomba hii mahakama iwaachilie washtakiwa hawa kwa masharti makali ya dhamana kwa vile wamefanya makosa mabaya kuliko ya kuua,” alisema naibu wa DPP Bi Emily Kamau.

Bi Kamau alimweleza hakimu mkuu mahakama ya kuamua kesi za ufisadi Bw Douglas Ogoti kuwa dhamana ni haki ya washtakiwa lakini akasema “washukiwa hawa walisababisha wagonjwa wengi kukata roho mahospitalini kwa kukosa pesa za matibabu.”

Washtakiwa walikanusha mashtaka 17 dhidi yao. Hakimu aliwaachilia kwa dhamana ya viwango mbali mbali kati ya Sh2milioni pesa tasilimu hadi Sh500,000 pesa tasilimu.

Bi Kamau alimsihi hakimu mkuu Bw Douglas Ogoti atilie maanani pesa zilizofujwa na washtakiwa hao 21 na kusisitiza,” wakenya waliofariki kutokana na

Walioshtakiwa ni aliyekuwa kinara wa NHIF Simeon Lemminte ole Kirgotty, aliyekuwa mkurugenzi mkuu Geoffrey Gitau Mwangi, wakili wa NHIF Ruth Sudoi Makallah, Pamela Nyaboke Marendi, Joseph Mutinda Mbuvi, David Muli Nzuki, Gibson Kamau Muhuhu, Irene Ng’etich Rono, Jacinta Nyakio Mwangi, Gilbert Gathuo Kamau, Kennedy Arthur Wakhu, Fredrick Sagwe Onyancha, Millicent Wangui Mwangi, Matilda Mwangemi, Darius Philip Mbogo, aliyekuwa mwenyekiti wa chama cha kitaifa cha kuwatetea walimu (KNUT) Mudzo Kuhenderwa Nzili , Yussuf Ibrahim, Elly Nyaim Opot, Danson Muchemi Njunji, Robert Muriithi Muna na kampuni ya Wentribe Limited.

You can share this post!

UFISADI: Raila awakosoa wandani wa Ruto

Hofu wafanyabiashara wakilipa wahuni kuua washindani wao

adminleo