• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
KRA yalenga kukusanya Sh2 bilioni kwa wenye biashara ndogo

KRA yalenga kukusanya Sh2 bilioni kwa wenye biashara ndogo

Na BERNARDINE MUTANU

MAMLAKA ya Kukusanya Ushuru nchini (KRA) inalenga kukusanya Sh2 bilioni kwa mwaka kutoka kwa wafanyabiashara wadogo.

Hii ni baada ya serikali kuanza kutekeleza ushuru mpya. KRA ilisema inashirikiana na simamizi za kaunti kuisaidia kukusanya ushuru huo unaolenga wafanyibiashara wadogo ambao hupata hupata chini ya Sh5 milioni kwa mwaka.

Wafanyibiashara wa jua kali wanafaa kulipa ushuru wa asilimia 15 ada ya biashara moja ambayo hutolewa na serikali za kaunti wanapoenda kufanya upya leseni zao kuanzia mwezi huu.

“KRA inalenga kukusanya Sh2 bilioni kufikia mwishoni mwa mwaka huu wa kifedha,” alisema kamishna wa KRA anayesimamia ubunifu na hali hatari Mohamed Omar.

Lakini huenda utekelezaji wake haujaanza vilivyo hasa kutokana na kuwa wafanyibiashara bado hawajui kuhusiana na ushuru huo.

You can share this post!

Mashirika ya serikali yadaiwa Sh1.9 bilioni na NCA

Wachina 3 wanaswa wakiwa na bidhaa haramu za wanyamapori

adminleo