• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 8:27 PM
BRAZIL: Pasta kutoka kuzimu

BRAZIL: Pasta kutoka kuzimu

NA MASHIRIKA

PASTA mmoja amekamatwa kwa madai ya kubaka waumini wake, baada ya kuwahadaa kuwa uume wake una ‘maziwa matakatifu’ ambayo wanahitaji ili wapone.

Bw Sobrino Valdeci Picanto, pasta kutoka Brazil anadaiwa kuwa aliwahadaa waumini hivyo kama mbinu ya kuhubiri neno, akisema ‘maziwa’ hayo ni matakatifu.

Pasta huyo anadaiwa kuwaambia waumini kuwa sehemu zake nyeti zimebarikiwa na kuwa “mungu ameziweka maziwa matakatifu ya roho mtakatifu’ na hivyo alitaka kuwapa.

“Alitwambia kuwa Mungu angeingia katika maisha yetu kwa njia yam domo tu,” akasema mfuasi.

“Mara nyingi baada ya ibada, pasta Valdeci amekuwa akitutaka kumfanyia ngono ya mdomo hadi roho mtakatifu aje na kuletea kanisa pesa,” akasema.

Pasta huyo wa miaka 59 alikamatwa alipokuwa eneo la Apore, Goias, nchini Brazil kwa kuwabaka wanawake kadha ambao ni waumini wa kanisa lake.

Aliwahadaa kuwa sehemu zake nyeti zimetiwa ‘mafuta matakatifu ya kiroho.’

Aidha, alidai kuwa alikutana na yesu katika soko la ngono, ambapo alimpa kazi ya kusambaza ‘manii matakatifu’ nchini kote, akianza na waumini wa kanisa la Apore ambalo huwa anahubiri.

“Valdecir aliopatikana peupe akipiga punyeto uume wake usoni mwa mfanyabiashara wa eneo hilo, kwa ahadi kuwa biashara yake ingenawiri baada ya kupata ‘mafuta hayo matakatifu.’

Kisa hicho kimetokea baada ya kingine Afrika Kusini, ambapo mhubiri mwingine naye alijeruhiwa vibaya na simba alipoenda kujianika mbele yao, akidai kuwa nguvu za roho mtakatifu zingemlinda. Aliokolewa na askari wa kulinda wanyama pori ambao walipiga risasi hewani kutawanya wanyama hao.

Wiki chache baadaye, mhubiri Mboro pia kutoka Afrika Kusini aliripotiwa kwenda mbinguni kwa mwili wakati ibada ilikuwa ikiendelea, kisha akarejea wiki moja baadaye na kudai kuwa alipiga picha za selfie na Yesu.

Amekuwa akiuza picha hizo kwa Sh50,000 moja. Aidha mhubiri huyo alidai kuwa Yesu ana mke Mwafrika ambaye ni mrembo sana, huko mbinguni.

You can share this post!

Mama amsamehe mumewe aliyemdhulumu kuokoa ndoa

PENZI LA MAUTI: Mume na mpango wa kando wazuiliwa kwa...

adminleo