Jeshi la Sudan lasema limezima shambulio la RSF
JESHI la Sudan limesema limezuia shambulio la wanamgambo wa RSF katika mji muhimu kusini mwa nchi hiyo Novemba 25, 2025 huku Amerika ikizihimiza pande zote mbili kukubali pendekezo la kusitisha mapigano.
Jeshi hilo lilizuia shambulio kwenye kambi yake katika mji wa kimkakati wa Babanusa ambao ni ngome yake kubwa katika eneo hilo.
Mapema Novemba 26, 2025, mjumbe wa Amerika barani Afrika, Massad Boulos, alisema akiwa Abu Dhabi kwamba pande zote hazijakubaliana na pendekezo jipya la kusitisha mapigano.
Pendekezo hilo liliandaliwa na kundi la Quad linalojumuisha Washington, Saudi Arabia, Umoja wa Falme za Kiarabu na Misri.