• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:33 AM
KRA yashauriwa kuwapa wawekezaji motisha

KRA yashauriwa kuwapa wawekezaji motisha

Na BERNARDINE MUTANU

Shirika la Kukusanya Ushuru nchini (KRA) limeshauriwa kuwapa motisha wananchi ili kuimarisha mapato kutokana na ushuru.

Hatua zinazovutia walipaji ushuru nchini zina uwezo wa kukuza tamaa ya kuwekeza katika utengenezaji wa viwanda, na kuimarisha nafasi za kazi.

Hali hiyo inaweza kuisaidia KRA kupata walipaji zaidi wa ushuru, kulingana na Mwenyekiti wa Wahasibu wa Umma Kenya (ICPAK) Julius Mwatu.

Kwa mfano, KRA inaweza kuwapa walipaji ushuru ‘likizo ya ushuru’na kuondoa ushuru unaotozwa mali ghafi inayoagizwa kutoka nje.

Kulingana na mwenyekiti huyo, waajiri pia wanaweza kupewa marupurupu kwa kuwaajiri wafanyikazi waliotoka shule juzi.

Alisema kuna haja ya kuwa na sera zinatia moyo wawekezaji lakini sio zinazowafukuza, kwa lengo la kuimarisha nafasi za kazi nchini.

You can share this post!

Idara yaomba mabilioni kujenga nyumba 500,000 za bei nafuu

Madereva wote kulipa Sh5,000 kupokea mafunzo mapya

adminleo