• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 5:55 AM
Kuria akataa marupurupu, aamuru pesa hizo zipelekwe Hospitali ya Gatundu

Kuria akataa marupurupu, aamuru pesa hizo zipelekwe Hospitali ya Gatundu

Na CHARLES WASONGA

MBUNGE wa Gatundu Kusini Moses Kuria Jumanne aliagiza usimamizi wa bunge kuelekeza pesa ambazo angelipwa kama marupurupu ya malazi kwa Hospitali ya Wilaya ya Gatundu.

Kwenye barua aliyomwandikia Karani wa Bunge la Kitaifa Michael Sialai Jumanne Bw Kuria alisema kuwa hatapokea sehemu yoyote ya pesa hizo zinazopendekeza kulipwa wabunge.

“Marupurupu haya hayana maana yoyote. Naishi katika nyumba yangu Nairobi na siwezi kushawishi familia yangu kuhusu ni kwa nini walipa ushuru wanapaswa kunilipa ili niwe mbali nao,” sehemu ya barua yake iliyoonekana na Taifa Leo Dijitali ilisema.

Bw Kuria pia aliweka nakala ya barua hiyo katika ukurasa wake wa Facebook.

Akaendelea kusema: “Naamuru kuwa ikiwa sharti nilipwe marupurupu, bunge lielekeze pesa hizo kwa Hospitali ya Wilaya ya Gatundu katika muda wote unaosalia katika kipindi change cha kuhudumu katika bunge la 12.”

Ufichuzi kwamba kuna mipango ya wabunge kulipwa takriban Sh24,000 kila siku kama marupurupu ya malazi katika siku ambazo wao huhudhuria vikao vya bunge umeibua kero kubwa miongoni mwa Wakenya.

Lakini mnamo Jumapili, Spika wa Bunge la Kitaifa Justin Muturi alitetea marupurupu hayo akisema yataimarisha moyo wa utendakazi wa wabunge kuwa kuwatia shime kuhudhuria vikao vya bunge.

Mnamo Jumatano iliyopita, wabunge walipitisha Mswada wa Huduma za Bunge inayopendekeza walipwe marupurupu kadhaa, yakiwemo ya malazi wakiwa Nairobi kuhudhuria vikao vya bunge ya kati ya Sh18,000 hadi Sh24,000 kila wiki.

Mswada huo sasa unasubiri kuwatiwa saini Rais Uhuru Kenyatta na hivyo kutoa nafasi kwa wabunge kufurahia mafao mengine kando na marupurupu kadha.

You can share this post!

Kangemi Ladies wahifadhi taji la NWRL

Mwanamke kulipwa Sh61m kwa kulazimishwa kujifungua akiwa na...

adminleo