• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 9:35 PM
Kizimbani kwa kupanga njama ya kushambulia makanisa

Kizimbani kwa kupanga njama ya kushambulia makanisa

Na RICHARD MUNGUTI

MSHUKIWA wa ugaidi mwenye umri wa miaka 19 anayedaiwa alikuwa amepanga njama za kushambulia makanisa matatu moja ya Salvation Army jijini Nairobi alifikishwa kortini Jumanne.

Trevor Ndwiga Nyaga aliagizwa azuiliwe hadi Desemba 18, 2019 mahakama itakapoamua ikiwa ataachiliwa kwa dhamana au la.

Ombi la mshtakiwa azuiliwe liliwasilishwa na kiongozi wa mashtaka aliyeeleza mahakama mshtakiwa alikuwa ametoroka lakini polisi wakafaulu kumptia nguvuni.

Hakimu mkazi Bi Muthoni Nzibe alifahamishwa mshtakiwa alikuwa amepanga kutorokea nchini DRC Congo baada ya kutekeleza shambulizi dhidi ya Kanisa hilo la Salvation Army.

Mahakama iliambiwa baada ya mshtakiwa kutiwa nguvuni alikutwa na nakala za maandishi ya ugaidi ikiwa ni pamoja na yale ya ukataji watu vichwa.

“Mshtakiwa alikutwa akiwa na kisu maalum kilichodhaniwa kuwa cha kutekeleza uhalifu,” hakimu alifahamishwa na kiongozi wa mashtaka.: Hakimu alifahamishwa kwamba mshtakiwa alikutwa amehifadhi nakala nyingi za vitabu vya kuendeleza ugaidi.

Mahakama iliombwa imzuilie mshtakiwa kwa wiki mbili kuwezesha polisi kukamilisha mahojiano na mashahidi.

Mshtakiwa alikana shtaka moja la kupatikana na mali iliyodhaniwa aliitazamia kuitumia katika visa vya uhain

Pia alikutwa na nakala za ugaidi zikihimiza wahanga wakatwe vichwa

You can share this post!

Korea Kaskazini yaahidi Trump ‘zawadi ya Krismasi’

Asimulia mahakama alivyoleweshwa na kubakwa usiku kucha na...

adminleo