• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 6:55 AM
Coronavirus: Mambo ya kutilia maanani

Coronavirus: Mambo ya kutilia maanani

Maambukizi na Vifo

KUFIKIA jana watu zaidi ya 82,000 walikuwa wamethibitishwa kuambukizwa coronavirus ambapo zaidi ya 2,800 walikuwa wamekufa na wapatao 33,000 wamepona.

Nchi zinazoongiza kwa maambukizi kufikia jana ni China (78,000), Korea Kusini (1,500), Italia (470), Japan (189) na Iran (139).

Dalili

Dalili zake zinategemea na hali ya afya ya mgonjwa. Lakini kwa kawaida huanza kwa joto jingi mwilini ikifuatwa na kikohozi kikavu. Baada ya wiki moja inasababisha matatizo ya kupumua.

Madaktari wanasema dalili kama makamasi, kupiga chafya na vidonda vya koo sio kawaida kwa wanaougua maradhi haya.

Kwa wazee na watu walio na maradhi yasiyo na tiba, dalili kama za numonia, uchungu kifuani na kuzimba pamoja na kushindwa kupumua zinajitokeza.

Walio hatarini zaidi

Watu walio na maradhi yasiyo na tiba wamo kwenye hatari zaidi ya kuambukizwa coronavirus na kufariki. Maradhi haya ni pamoja na mkimbio wa damu, matatizo ya moyo, kisukari na matatizo ya kupumua.

Muda wa kujitokeza

Baada ya kuambukizwa, dalili huanza kujitokeza kwa kati ya siku 2 hadi 14. Hata hivyo kumekuwepo na visa vichache ambapo dalili zinaonekana baada ya siku 19 hadi 27.

Hatari ya kufa kulingana na umri

Wazee ndio wamekufa zaidi kutokana na coronavirus.

You can share this post!

Mataifa ya kigeni yanavyokabiliana na coronavirus

Kongamano kuhusu tabia-nchi kufanyika Makueni

adminleo