• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 3:10 PM
Serikali yahakikishia wawekezaji sekta ya utalii kwamba inawapima wageni wote wanaoingia nchini kwa ndege

Serikali yahakikishia wawekezaji sekta ya utalii kwamba inawapima wageni wote wanaoingia nchini kwa ndege

Na WINNIE ATIENO

SERIKALI kuu imewahakikishia wawekezaji katika sekta ya utalii kwamba inaweka juhudi kukabiliana na virusi vya corona ili kuzuia maambukizi kutoka nchi za kigeni baada ya kufunguliwa kwa viwanja vya kimataifa vya ndege.

Mkuu wa idara ya afya ya umma katika Wizara ya Utalii, Bi Susan Mutua, alisema serikali inajizatiti kukabiliana na tishio la maambukizi ya kigeni kutoka kwa wageni wanaoingia humu nchini kupitia viwanja vya kimataifa vya ndege na madereva mipakani.

Mnamo Agosti 1, 2020, serikali ilifungua rasmi viwanja vya kimataifa vya ndege, huku wawekezaji katika sekta ya utalii wakijizatiti kutafuta watalii baada ya soko hilo kudorora kwa sababu ya janga la corona.

Nchi nyingi bado hazijawaruhusu raia wake kusafiri nje kufuatia janga la corona.

Hata hivyo, Bi Mutua alisema serikali ya Kenya sasa inakabiliana na maambukizi ya virusi vya corona miongoni mwa wanajamii – community infection – na kwamba maambukizi kutoka raia wa kigeni ni machache.

“Tunapima wale wote wanaoingia humu nchini kupitia mipaka yetu na hata wale wanaotumia wnja zetu za kimataifa, ili kuzuia usambaa wa virusi kutoka nchi za kigeni. Ni sharti wageni wote wapimwe hususan madereva wa bodaboda wanaoigia humu nchini kupitia mikapa yetu ili kuzuia virusi kutoka nchi za kigeni,” alisisitiza.

Haya yanajiri huku wawekezaji wa sekta ya utalii wakiwa na matumaini kwamba utalii utaimarika endapo virusi hivyo vitapungua. Hata hivyo waliwaisihi serikali kuuza soko la Kenya ughaibuni ili kupata watalii wengi kuzuru eneo hilo.

Kwa sasa wadau wa sketa ya utalii wanategemea utalii wa humu nchini.

Mwenyekiti wa Shirikisho la Utalii nchini, Bw Mohammed Hersi na mwenzake wa muungano wa pwani wa wakezaji wa utalii Bw Victor Shitakha walisema kufunguliwa kwa viwanja vya ndege za kimataifa kutaimarisha utalii.

“Tangu kufunguliwa kwa viwanja vya kimataifa wa ndege, sekta ya utalii imeanza kuimarika huku tukipata wageni wachache eneo la pwani. Lakini bado tuko asilimia 20 kwa idadi ya vitanda; wakati wa wikendi huwa tunapata wageni asilimia 50-60 kwa hoteli zingine kupitia utalii wa humu nchini,” alisema Bw Shitakha.

Bw Hersi naye alisema kufunguliwa kwa viwanja hivyo fufuo la tumaini kwa utalii.

“Gazeti la Forbes lilitaja Kenya kuwa miongoni mwa nchi tisa ambazo ziko tayari kupokea wageni. Hii ni habari njema kwa sekta yetu. Janga la corona limeathiri dunia nzima lakini tunafaa kuweka mikakati kufufua sekta yetu,” alisisitiza Bw Hersi.

You can share this post!

Fundi wa majahazi anayeunda mashua na mitumbwi

ONGAJI: Serikali ijitolee kikamilifu kuwalinda raia walioko...