• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Huenda City Hall ikaadhibiwa vikali na Kenya Power

Huenda City Hall ikaadhibiwa vikali na Kenya Power

Na BERNARDINE MUTANU

HUENDA serikali ya kaunti ya Nairobi ikakatiwa umeme na kampuni ya Kenya Power kutokana na bili kubwa.

Mahakama Jumatano iliipa Kenya Power ruhusa ya kuitisha Sh732 milioni inazodai Serikali ya Kaunti ya Nairobi.

Ikiwa serikali hiyo haitalipa pesa hizo, Kenya Power ilipewa ruhusu ya kukatia serikali hiyo umeme.

Kulingana na Jaji John Mativo, serikali ya Kaunti ya Nairobi ilipoingia mamlakani ilikubali kutwaa madeni yote ya Baraza la Jiji la Nairobi.

Serikali ya Evans Kidero ilienda mahakamani kupiga kutozwa bili hiyo kwa kusema iliachwa na NCC.

You can share this post!

Sonko apinga kesi ya Sh1.7 bilioni

Mashabiki wa Gor wakejeli washambuliaji kwa kufuma mabao...

adminleo