• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 5:46 PM
Ni faida tu kwa benki ya Equity

Ni faida tu kwa benki ya Equity

Na BERNARDINE MUTANU

BENKI ya Equity imetangaza ongezeko la asilimia 22 ya faida baada ya kutozwa ushuru.

Kampuni hiyo ilipata faida ya Sh5.9 bilioni kutoka 4.9 bilioni mwaka uliotangulia.

Mwaka 2017, kampuni hiyo ilipata ongezeko la faida la asilimia 14 baada ya kutozwa ushuru wakati benki zingine zilikuwa zikitangaza hasara.

Faida hiyo ilitokana na ongezeko la wateja wapya 1 milioni na hivi sasa ina wateja 12.2 milioni ambapo pesa zilizowekwa na wateja wake ziliongezeka kwa asilimia tisa hadi Sh382.4 bilioni kutoka 349.3 bilioni, ilisema benki hiyo jana katika taarifa.

Kwa sasa Equity ina wateja 12.2 milioni.

You can share this post!

Serikali yajiondoa kwa biashara ya hoteli

Bomba jipya la KPC kusafirisha lita milioni 1 kwa saa

adminleo