Kimataifa

Mwanahabari Misri akamatwa kwa kuonyesha video ya maandamano

October 7th, 2020 Kusoma ni dakika: 1

NA AFP

Polisi wamekamata mwanahabari nchini Misri kwa kuonyesha video ya maandamano mjini Luxor,  amesema mwajiri wake na mwanasheria wake.

Basma Mostafa alifikishwa kortini Jumapili baada ya kupotea siku moja baada ya kuripoti kuhusu maandamano hayo kijijini Al-Awamya.

Alikamatwa alipokuwa akiripoti kuhusu mauaji ya mwanaumme aliyeuliwa na polisi wakati wa maandamano hayo kulingana na mwajiri wake ulisema mtando wa Al-Manassa.

“Pandey a mashtaka iliagiza mwanamke huyo abaki kizuizini kwa siku 15 wakigoja uchunguzi kuhusiana na mwanamke huyo kujiunga na kikundi haramu cha kigaidi na kueneza habari za uongo,” alisema mwanasheria wake Hala Doma kwenye ujumbe aliouandika kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook.

Mamia ya wananchi wa Egypt walifanya maandamano vijijini mwezi Septemba kulingana na video iliyosambaa mitandaoni sanasana waugaji mono wa dini la Kislamu.

Maandamano hayo yalikuwa yamejawa na hasira hasa kutoka kwa wakazi wa vijijini na maeneo yenye umaskini kuhusiana na mijengo inayohuhusiana na kampeni ya setikali.

TAFSIRI NA FAUSTINE NGILA