• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 5:54 PM
SAKATA YA NYS: Uhuru ategemea DCI, DPP kuliko tume ya EACC

SAKATA YA NYS: Uhuru ategemea DCI, DPP kuliko tume ya EACC

Na BENSON MATHEKA

RAIS Uhuru Kenyatta ameonekana kubadilisha mbinu za kupigana na ufisadi huku akihusisha Idara ya Upelelezi wa Jinai (DCI) na lile la ujasusi (NIS) kuliko Tume ya Maadili ya Kukabiliana na Ufisadi (EACC).

Hii inadhihirika katika uchunguzi wa sasa wa sakata mbali mbali za ufisadi ambapo Mkurugenzi wa Upelelezi wa Jinai George Kinoti aliwasilisha faili za uchunguzi wa kashfa ya wizi wa Sh0.5 bilioni kwa Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma DPP moja kwa moja.

Jumanne, DPP Noordin Haji hakutaja EACC kwenye taarifa yake kuhusu washukiwa wa sakata ya NYS waliokamatwa na wanaochunguzwa.

Awali kwenye barua, Mkuu wa Utumishi wa Umma Joseph Kinyua alimwambia Bw Kinoti kwamba Rais alitaka mashirika yote kushirikiana katika uchunguzi.

Kinachoonyesha kwamba EACC halikuhusishwa kikamilifu ilivyokuwa kwenye sakata ya kwanza ya NYS 2015, tume hiyo haikutumiwa nakala ya barua hiyo.

Kwenye barua hiyo Kinoti na Haji waliagizwa kuwa wakimwarifu Rais kila siku kuhusu hatua za uchunguzi. Kashfa ambazo DCI inachunguza ni yaa NYS, Kampuni ya Mafuta na Kenya Power ambayo inasikisiwa kuwa Wakenya walipoteza zaidi ya Sh10 bilioni.

Na Wadadisi wanasema kuwa rais anaonyesha ana imani na maafisa wa DCI chini ya Bw Kinoti kuliko EACC ambalo limekuwa likijivuta kufanya uchunguzi.

 

 

 

 

You can share this post!

SAKATA YA NYS: Mianya ndani ya mfumo wa IFMIS yalaumiwa kwa...

Wetang’ula atisha kutoboa siri zote za Raila Odinga

adminleo