• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 7:55 PM
Jambazi amvunja shingo ajuza wa miaka 100 kisha kumuibia

Jambazi amvunja shingo ajuza wa miaka 100 kisha kumuibia

Na MASHIRIKA

DERBY, UINGEREZA

JAMBAZI alimshambulia mjane mkongwe mwenye umri wa miaka 100 na kumjeruhi vibaya alipokuwa akienda kanisani.

Ripoti zinasema Bi Sophia Kaczan alishambuliwa ghafla akavunjwa shingo na kupokonywa mkoba wake.

Ilisemekana alijikokota mwenyewe baada ya shambulio hilo na kuendelea kutembea hadi kanisani ambako alitafutiwa usaidizi.

Polisi walinukuliwa kusema majeraha aliyopata hayahatarishi maisha yake na wakatoa wito yeyote aliyeshuhudia kisa hicho ajitokeze kuwasaidia kusaka jambazi huyo.

Majirani wake walihuzunishwa na kisa hicho wakasema huenda aliyemshambulia alikuwa akitazama mienendo yake kwa muda mrefu. Hata hivyo, ilisemekana mkoba huo haukua na pesa.

You can share this post!

Waziri na wabunge 13 watoa Sh1,216 pekee kwa mchango

Sungura 27 wahangaisha maafisa katika kituo cha treni

adminleo