• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:33 AM
Kasisi motoni kwa kupora wanawake Sh1.3 milioni

Kasisi motoni kwa kupora wanawake Sh1.3 milioni

Na RICHARD MUNGUTI

MSHUKIWA aliyejitambulisha kwa kikundi cha kina mama kuwa Kasisi wa kanisa la Kianglikana na kupokea zaidi ya Sh1.3milioni Jumatatu alishtakiwa kwa kuwadanganya angeliwasaidia kununua ardhi katika eneo la Kitengela kaunti ya Kajiado miaka sita iliyopita.

Bw Gordon Apora Anyumba aliyefikishwa mbele ya hakimu mkuu Mahakama ya Milimani Nairobi Bw  Francis Andayi alikanusha shtaka la kuwatapeli kina mama hao Sh1,350,000.

Shtaka lilisema kuwa kikundi hicho cha kina mama kinajulikana kwa jina Lima Women Group.

Kiongozi wa mashtaka Bw Solomon Naulikha , alisema Bw Anyumba alijitambulisha kwa kikundi hicho cha kina mama kuwa Kasisi wa Kanisa la Anglican Church of Kenya (ACK) anayehudumu katika kanisa la St Stephens tawi la Jogoo Road Nairobi.

Bw Naulikha alisema mshtakiwa alikuwa anakutana na wanachama 13 wa kikundi hicho cha kina mama katika kanisa hilo la ACK tawi la Jogoo akidai ardhi aliyokuwa anawasaidia kina mama hao kununua inamilikiwa na kanisa hilo la ACK.

Mahakama Ilifahamishwa kuwa mshtakiwa aliopkea pesa hizo kutoka kwa kundi hilo la kina mama waliokuwa wanataka kuekeza katika mradi wa ujenzi wa nyumba kati ya Agosti 24 na Novemba 14 2012.

Mshtakiwa alikanusha shtaka hilo na kuomba aachiliwe kwa dhamana.

Bw Naulikha hakupinga mshtakiwa akiachiliwa kwa dhamana.

Bw Andayi alimwagiza mshtakiwa awasilishe dhamana ya pesa tasilimu Sh300,000 na kutengeza kesi hiyo isikizwe  Agosti 21 mwaka huu.

Mahakama pia iliamuru mshtakiwa akabidhiwe nakala za ushahidi ulionakaliwa na polisi.

You can share this post!

TUZO YA NOBEL: Sheria ambazo Raila anafaa kufuata kushinda...

Makumbi aonyeshwa mlango na Western Stima

adminleo