• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 9:50 AM
Afueni kwa mabinti 22 wa UG walionaswa Kenya wakisafiri Dubai

Afueni kwa mabinti 22 wa UG walionaswa Kenya wakisafiri Dubai

Na RICHARD MUNGUTI

MAHAKAMA imefuta mashtaka dhidi ya wasichana 22 raia wa Uganda waliotiwa nguvuni Kenya wakiwa na paspoti feki za usafiri.

Washtakiwa hao walikuwa wanajaribu kusafiri hadi Dubai kutafuta ajira walipotiwa nguvuni na maafisa wa idara ya uhamiaji.

Kiongozi wa mashtaka kutoka idara hiyo Bw Mutelo alimweleza hakimu mkuu mahakama ya Milimani Nairobi  Bw Francis Andayi kuwa pasipoti za washtakiwa zilikuwa na Visa zilizoghushiwa.

“Mbona mmetengeneza cheti kimoja cha mashtaka,” Bw Andayi alimwuliza Bw Mutelo na kuongeza , “ Ushahidi uko wapi utakaoniwezesha kuwapata washtakiwa na hatia.”

Mahakama ilikataa mashtaka yaliyotayarishwa na maafisa hao na kuamuru washtakiwa warudishwe rumande na kuagiza kila mmoja ashtakiwe peke yake.

You can share this post!

DPP aitisha faili ya askari jela aliyemuua mwanachuo

Kesi ya Mutua kuamuliwa Agosti 6

adminleo