• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Wachumba wamwagiwa kinyesi kwa kula uroda nje ya ndoa

Wachumba wamwagiwa kinyesi kwa kula uroda nje ya ndoa

Na MASHIRIKA

LANGSA, INDONESIA

WAPENZI wawili walimwagiwa kinyesi kwa kudaiwa kushiriki ngono nje ya ndoa zao katika eneo la Langsa, Indonesia.

Video iliyosambazwa mitandaoni ilionyesha umati wa watu ukiwavuruta mwanamume na mwanamke wanaoonekana kuwa wenye miaka ya thelathini na kuwapeleka kando ya shimo la maji taka.

Walikalishwa hapo kisha umati ukaleta ndoo ambazo zilitumiwa kuchota maji hayo yenye uchafu wa kila aina ikiwemo kinyesi, na kuwamwagia vichwani na mwilini.

Nchini humo wakazi wengi hufuata sheria za Kiislamu na hivyo basi ni haramu kwa watu kutenda ngono nje ya ndoa.

Ripoti za habari zilisema mwanamume huyo ni mkubwa wa idara ya kiserikali na mwanamke husika ni mwajiriwa wake.

Ilidaiwa mwanamume huyo alikuwa akienda nyumbani kwa mwanamke mara kwa mara, na wakazi waliwachunguza mienendo yao kwa muda kabla kuwanasa.

Ilisemekana wawili hao walijitetea na kusema walioana kwa njia ya kidini lakini umati ukaendelea kuwaadhibu.

Walichukuliwa na polisi baadaye ambao walinukuliwa kusema watafanya uchunguzi zaidi na ikiwa itabainishwa kwamba cheti chao cha ndoa ni feki, huenda wakaadhibiwa kisheria kwa kuchapwa mijeledi hadharani.

-Imekusanywa na Valentine Obara

You can share this post!

Alilamba vya pembeni, sasa hana ‘transfoma’...

TUNARUDI TENA CHAMA KIMOJA? Demokrasia hatarini

adminleo